ONGEZEKO LA WIMBI LA NGONO KATIKA JAMII
YETU NINI TATIZO?
Hili tatizo sio nchini kwetutu bali limetapakaa
ulimwenguni mwote ila kila sehemu kwa namna yake athari zake hazifanani wala
vyanzo havifanani.
Kama ni mtanzania ambaye unaipenda nchi yako na
unaifwatilia katika majanga mbalimbali ambayo nchi yetu inakumbwa katika kipidi
hiki tulichonacho moja wapo ni uongezeko la vitendo vya ngono katika jamii
tuliyo nayo na matokeo yake kusababisha madhara mbalimbali.
Ongezeko hili ni hatari kwa kuwa alina matokeo
mazuri katika jamii tuliyo nayo katika Nyanja zote kijamii,kiuchumi na hata
kisiasa zaidi sana kuchochea maendeleo kushuka katika jamii husika.
Japo wako watu wanafaidika kutokana na jambo hili
hivyo mawazoni mwao ni kwa jinsi gani kuhakikisha jambo hili litazidi kukua na
kukubalika katika jamii yote kwa ujumla.
Hivyo kuna mashindano ndani ya jamii moja wako watu
ambao wanapenda jambo hili liendelee na wako watu ambao wanapenda jambo hili
likomeshwe, pamoja hayo jambo hili alijahusisha watu wenye hali ngumu ya uchumi
tu bali pia na hata watu ambao hawajui maana ya njaa au shida hivyo sio jambo
utalifikiria kwa muda tu alafu ukalipatia utatuzi wa kudumu.
Jambo hili kwa watu wanaoshiriki wanaona wako sawa
kutokana na sababu mbalimbali watakazo kukueleza na wengi wao wakisema hali
mbaya/ngumu ya uchumi katika maisha.
Lakini ikiwa mtu ambaye unajielewa na kujithamini
zaidi sana wazazi wenye akili nzuri na watoto wao hawafurahii jambo hili
linapotendeka hasa likiwahusisha watoto wao au watu ambao wanao wapenda.
Ngono hivi sasa katika jamii yetu limekuwa ni jambo
ambalo lisilo na heshima lilowazi ambalo akuna mficho tena katika jambo hili.
Hivi sasa unaweza kuamua leo kufanya ngono muda
wowote na wakati mwingine kwa mtu unaye mtambua ambaye yuko tayari au kwa mtu
ambaye umtambui lakini vilevile naye lazima awe tayari.
Kwa jamii tuliyo nayo sasa jambo ngono alina rika
maalumu kwamaana sasa hata wanafunzi wa shule za msingi wanafahamu vizuri zaidi
sana nao wanashiriki kuhusika na jambo hili au mahali maalum ila ni popote
ambapo mtakubaliana au mmoja atapenda kushiriki swala hilo.
Katika jamii wako watu watu waliingia kutokana na
msukumo mbalimbali baadae wakajuta na hata kujaribu kuhusia kwa watu wengine
wasije kujiingiza katika hii biashara haramu lakini matokeo yake jambo hili
linazidi kushika hatam siku baada ya siku.
Jambo hili limekuwa na sura yakutisha sasa ambayo
imeota sugu, kama mti basi mizizi yake imekwenda mbali sana ambao ili kung’oa
sio swala la mchezo tu.
Jambo hili limeleta matatizo katika jamii pindi
linapozidi kuongezeka basin a athari zake zimekuwa zikishamiri kwa kiasi
kikubwa;
i.kifo
wako watu kutokana na kutendwa na wenzi wao
iepelekea kufa, kwa sababu kukosa kujua nini cha kufanya, japo hakuna mtu
anaweza kuona nijambo lililo gumu sana mpaka kufikia hatua hiyo ya kujiua
lakini limeshatokea katika jamii na bado linaendelea kutokea.
Japo unaweza kusema kifo ni mpango wa Mungu lakini
jambo hili limekuwa likileta utata katika jamii yetu kwa kupoteza watu ambao
tulio wapenda wanaweza kuwa wazazi,rafiki,ndugu wakaribu sana hata wako watu
ulio wapenda na kuwaheshimu na kuwa thamini lakini kifo kimewatenganisha pasipo
kutimiza yaliyo malengo yenu.
ii.kupoteza
thamani ya ndoa
ndoa watu wakiishi kwa kujiami na kwa hofu kuu na
sio kwakuona fahari ya kuwa huyu ni wangu na huyu si wa watu wengine. Watu
wanaingia kwenye ndoa wakiwa na mawazo mengi kuona tutadumu kweli
je!tutafurahia ndoa yetu je! Moyo wangu hautajeruhiwa je! Maisha haya hayatanithiri
kwa magonjwa.(shinikizo la damu,magonjwa ya ngono mfano.kaswende)
Waku hawana imani na wenzi wao pindi wanapo kwenda
kazini,mashuleni na hata anapo pewa safari ya kikazi mashaka yanatawala maisha
yake.
Neno kuwa niko tayari kuolewa au niko tayari kukuoa
limekuwa likipokelewa kwa furaha lakini baadae uja na kuona ili neno lina
maanisha kama linavyo tamkwa.
Hata walio katika ndoa wako watu wanafanya ngono na
wasio wenza wao wengine wanafanya ndani ya nyumba na wengine mbali na makazi ya
mwenzi wao.
Japo katika ndoa kuna sababu mbalimbali
zinazopelekea hali kama hii lakini mwisho wa siku kunakuwa hakuna heshima
katika ndoa na watu wengine hawataiheshimu kwa sababu ninyi wenyewe hamuipi
heshima inayotakiwa.
iii.magonjwa
ya zinaa
wako watu katika jamii yetu wanawalaumu wenzi wao
kwa magonjwa waliyo yapata na kupelekea mateso ambayo wanaishi nao.
Kutokana na magonjwa haya ya ngono yanaathari
mbalimbali mathalani kifo,kupunguza ufanisi katika kazi na hata kupelekea
msongo wa mawazo, haya mambo haya yana sababishwa sana na wenzi wasio waaminifu
lakini athari zake upelekea kwa wote wanaomzunguka.
Kuna mfano ambao niliosimuliwa na moja wa athirika
hao katika ndoa:
Mama mmoja yeye aliye jitunza na kuthamini ndoa yake
katika hali zote alidhamilia kuiheshim ndoa yake na kumjali mume wake kwa namna
yoyote, siku moja mume wake alikuwa katika shughuli zake za kawaida kwakua
alikuwa dereva wa magari ya mizigo akisafirisha mizigo kutoka sehemu mmoja na
kwenda sehemu nyingine na hata wakati mwingine ilikuwa kutoka nchi moja na
kwenda sehemu nyingine. Siku si nyingi mwanamke akapatwa na maradhi katika
mwili wake na pindi alipoenda hospitalini kupata matibabu zaidi alijikuta
ameathirika na virusi vya ukimwi na ndipo dhamira yake ikaanza kuyachunguza
maisha yake na mwisho ukabani ni mume wake atakuwa amehusika ndipo walipokwenda
nyumbani na kufanya majadiliano na mwenzi wake ndipo mwanaume alipogundua
alishawai shiriki na wanawake wengi katika katika kufanya mapenzi na kukiri
kuwa ugonjwa huo ameuleta yeye nyumbani sawa na dhamira yake ilivyokuwa
ikimshuhudia.
Mwanamke huyu katika maisha yake alikuwa akimlaumu
mume wake siku zote.
Hili nijambo ambalo lilikuwa ni fundisho kwangu na
machozi ya Yule yalikuwa ni maneno yakisema ndani ya moyo wangu.
iv.moyo
kujeruhiwa
hii ni kawaida kwa mtu aliyeshiriki tendo la ndoa na
wewe kwa raha na huku wote mkifurahia ghafla ukakuta kunaanza kuwatofauti na
vile mwanzo mlivyo kuwa inaweza kuwa katika muda kuwa mfupi katika kufanya
tendo hilo au siku za kufanya tendo hilo kupunguwa kama mtu mwenye akili timamu
kutakuwa na maswali mengi ambayo utakayo ukijiuliza kwa nini hali kama hii,
bila shaka utaanza kujichunguza na kutaka kujua mapungufu ni yapi au nini
umemboa au ulicho muuzi na pindi unapokosa jibu
moyo wako unakuwa nyong’onyea.
Na hali hii inapoendelea ndivyo moyo wako unazidi
kujeruhiwa hatiamae kufikia kipindi kufanya yale ambayo hapo mwanzo
ukuyafikiria kuyafanya.
Kidonda ndani ya moyo wako kuja kupona sio jambo la
kawaida kinahitaji uwazi uliokuwa wa kweli ilikiweze kupona.
Moyo uliovunjika matokeo yake ni shinikizo la
moyo,vidonda vya tumbo na maradhi ya mifupa pamoja na mengine mengi.
v.watoto
wa mitaani
katika swala zima la ngono watoto wengi wanazaliwa
katika maeneo yasiyo rasmi upelekea kukataliwa na hatimae kujitafutia maisha
yao binafsi katika kudhi mahitaji yao.
Hakuna mtu anapenda haya matokeo lakini katika tendo
hili watoto wanamna hii uweza kutokea na hatimae kupelekea ongezeko la watoto
wamitaani, japo si wasemi vibaya watoto hawa wengine wasio na maadili upelekea
unyang’anyi na upolaji katika mitaa.
Japo sio hawa tu wanafanya vitendo hivi ni watoto wa
mitaani bali hata watoto wasio wa mitaani nao wameshiriki katika vitendo hivi
vya uporaji na unyang’anyi.
Pamoja zipo athari nyingi zinazotokana na ongezeko
hilo la ngono ndani ya familia,jamii na katika nchi kwa ujumla wake.
Tuone nini tatizo hatimae kupelekea uongezeko hili
kuongezeka kwa kasi tena katika namna mbalimbali kwa uwazi mkubwa.
UTU KUKOSA THAMANI
Kwa upande wangu ninaona tatizo hili la ngono
kuongezeka ni kukosa kuthamani utu wako binafsi japo kuna sababu mbalimbali
kila mtu ukimuuliza kwa nini umeamua kushiriki mtandao huu wa ngono wengi
watasema hali ngumu ya maisha,kusalitiwa na wenzi wao na nyingine nyingi.
Lakini mimi naomba nijikite katika hili watu kukosa
kuthamini utu wao binafsi upelekea watu kuto kukuthaminiwa.
Unaweza kuwa mtu yeyote ni vile utaamua kujithamini
na kuweka bidii katika kile unachokitalajia kuweka bidii kama utajithamini ni
ngumu kukubalika katika maeneo yote ila unaweza kukubalika maeneo Fulani na
mengine usikubalike. Hivyo kushindwa kufikia lile ambalo ulikuwa ukitegemea
kuwa utafikia.
Ni vizuri utambue kuwa hakuna mtu ambae atakuthamini
zaidi wewe unavyo jithamini binafsi.
Ni vizuri utambue utu wa mtu hauwezi badilishwa na
chochote hakuna thamani yeyote unaweza kubadilisha na utu wa mtu akipo wala
hakuna kitachotokea.
Tambua
utu wako ndio thamani yako, utunze ili uweze kuendelea
kuthaminiwa.
Ishi maisha ya kupandisha thamani yako siku baada ya
siku na sio kupunguza thamani siku baada ya siku, wewe ndio mwenye hatima yako
na wala hakuna mwingine ataweza kuchukua thamani yako.
Imeandaliwa na;
Nelson, Cothey – 0764 018
535 or cotheyn@yahoo.com
Katiti, James - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com
“BARIKIWA……….sana”