Jumamosi, 11 Januari 2014

MSAMAHA NI ZAIDI YA NENO



MSAMAHA

Hili ni moja ya jambo  muhimu sana katika maisha ya mwanadamu mahali ambapo anakosewa anapenda aambiwe samahani na mahali anapokosea anabudi kuomba msamaha na katika haya yote mawili 

kunakukubaliwa na kukataliwa pia kuna hali ya kukubali au kukataa, japo mtu yeyote anayeomba msamaha kutoka moyoni hasa pale anapoona kweli amekosa utazamia kusamehewa na hali ya mwanzo kurudi tena. 

Na yule anayesamehe anategemea jambo lililotendeka alitajirudia tena na itakuwa amejifunza kutokana na makosa.

Jambo hili sio swala la kuzoelea kwakua ni jambo ambalo linatokana na mtikisiko ndani ya mausiano yenu na kuhatarisha mmomonyoko wa hali ya kuhusiana kwenu japo wakti mwingine inasababisha hali ya kujuana zaidi na kutambua tofauti zenu na mapungufu yenu na kujua kuwa kuwa huyu yuko hivi na wala si hivi nilikuwa nikifikiria.

Na mtu ambaye hawezi kuomba msamaha wakati kweli amefanya makosa basi ni mtu anayetambulika kuwa anakiburi na ajali maumivu ya wengine na haoni uhitaji wa mwingine katika maisha yake hivyo jamii kwa mapana yake umchukulia kuwa ni mtu ambaye anayeweza kuanguka wala hata dawa(ataangamia).

NINI  MAANA  YA  MSAMAHA,

(a)    Msamaha ni ni hali ya kumbeba kristo ndani ya moyo wako pasipo kuangalia/kuruhusu mwanadamu au kundi la watu au mtu mmoja anataka/wanataka kubebwa ndani ya moyo wako.

-ukweli jambo lolote ambalo linakuumiza basi linapeleka kitu kutuama ndani ya moyo wako lakini ni hali ya kuzuia kwa jambo lolote lisipate nafasi ndani ya moyo wako basi liwe na sehemu nyingine lakini si katika moyo wako binafsi inaweza kuwa katika akili yako na ikapata ufafanuzi na ikaishia hapo.

-msamaha ni ishara ya kumpenda Mungu kuwa kitu ambacho kizunguke ndani ya moyo wako sikuzote, mambo ambayo Mungu atayafurahia akiyaona yakizunguka ndani yako siku zote kwa ubora na ustawi wake tu.

-unapoamua kusamehe ukweli ni kwa faida yako kwakua unaiweka huru nafsi yako mbali na mgandamizo pamoja na msongo wa mawazo ndani yako na hatimae kutofanikisha au kutikuwa na hali ya utendeaje ulikatika ufasaha.

 Mithali 4:23
-utaweza kuulinda moyo wako endapo tu utafanikiwa kwa kiwango cha juu cha kristo kukaa ndani yako na kupata nafasi inayostahili, kwa kua yeye ukimpa moyo wako atautunza moyo wako kuhakikisha haujeruhiwi kwakua ukijeruhiwa yeye atafurahi kukaa na wewe katika hali ya moyo kuwa chini au moyo wenye hofu.
Lazima utambue pindi utakapo mbeba mtu badala ya Mungu ndani yako basi utaongzwa na mtu lakini ujue hakuna hatima yako iliyo bebwa na mtu mwingine isipokuwa Mungu tu.

(b)   Msamaha ni hali ya kukubali kuonekana sawa mbele za Mungu na huku aliye kukosea au uliyemkosea akaona hana sababu ya kuomba msahama

Mithali 19:11

Warumi 8:13

-usifanye kitu ambacho kitaleta faida kwa mtu tu au hasara bali kile kitu kitakusaidia kusonga mbele zaidi ambacho kitakupa kibali zaidi mbele Mungu.

-hakuna njia nzuri ya maendeleo ikiwa tu utendaji wako unategemea nitawafurahishaje watu ili nisionekane mbaya, bali tambua kukuona mbaya au mzuri inategemea mitazo yao kwako na kamwe hauwezi kuibadilisha kwa namna yeyote bali fanya jambo ambalolitakupa usahihi mbele za Mungu.

-watu hawawezi kukuelewa kwa kua hata wao hawajielewi na zaidi ya yote hata wewe bado unajielewa siku zinavyozidi.



imeandaliwa na ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com




Ni  vizuri  kusamehe  ili  usamehewe……..

Jumatano, 8 Januari 2014

TAMBUA MSAMAHA NA MAZINGIRA YAKE

MSAMAHA NA MAZINGIRA YAKE;


Kila kitu duniani ilikiende vizuri lazima pawepo na hali ambayo itasindikiza tendo/jambo hilo kutokea kwa ukamilifu wake, jambo ambalo alitasindikizwa na hali stahiki jua kitu hicho hakita kuwa na nguvu katika utendaji wake.

Kila kitu nguvu yake utegemea sana hali gani inayoisukuma jambo hilo litendeke pasipo hali hiyo jambo hilo linakuwa alina nguvu.

Tunapozungumzia hali ya kukufanya utende jambo tuna zungumzia shina ulilonalo katika utendaji wa jambo husika ambalo linakupa nguvu katika utendaji wake.

Mfano unapokuwa na furaha je, hali gani uliyonayo inayo sindikiza hicho kicheko kama hali inayokusindikiza katika kicheko sio sahihi basi hicho kicheko kinaweza kuitwa ni unafiki na hata unapolia je, haligani inasindikiza katika kilio chako napindi hali uliyo nayo ikatofautiana na hali uliyokuwa nayo basi uweza kuitwa ni unafiki.

Jambo lolote ili liwe imara utegemea sana shina la jambo hilo kwa hiyo uimara wa shina upelekea ubora wa jambo husika….kwakua uimara wa nyumba utegemea msingi wake na ubora wa mti utegemea sana mizizi yake.

Jambo lolote hili ulifanye katika ubora wake unahitaji sana ujue kwa ufasaha zaidi kwa nini nafanya jambo hili unapojua basi pajenga umaana wa wewe kufanya jambo hilo.

MSAMAHA limekuwa neno la kawaida katika jamii yetu inayotuzunguka, hakuna mtu hajawai kulitumia hili neno(katika maana ya kuambiwa au kusema) watu imefika wanachoka kusikia neno hili.

Hili neno limekuwa likitumika sana hatakufika mahali ambapo kushindwa nani ana maanisha na nani amaanishi imekuwa ikiwa katikati inaweza kumsamehe huyu kumbe huyu amefanya makusudi na unaweza usi msamehe huyu kumbe huyu akufanya kwa makusudi ki uhakika hili neno limekuwa liki wachanganya watu sana kwa watu wako njia ya panda hawajui wafanye nini bali wamekuwa wapweke kwa kutojua nifanye nini.

Kila mtu anakuwa na maamuzi yake pindi anapotaoa msamaha wake mwingine atasema nimekusamehe lakini usirudie tena,mwingine usema nimekusamehe lakini sitaki kukuona ukifanya jambo lilelile tena na kuwa na mtu Yuleyule tena,mwingine atasema nimekusamehe lakini sitaji tena kukuona katika maisha yangu tena, mwingine atasema nimekusamehe ila hama mahali hapa au mimi na wewe tutengane tusiwe pamoja tena na mwingine atasema nimekusamehe ila tufanye mapenzi mimi nawe ili tuyamalize kabisa au tumalize tofauti zilizopo kati yetu, au mwingine atasema nimekusamehe ila sasa utakuwa ukifanya hivi au utakuwa ukinifanyia hivi.

Haya yote ni mazingira mbalmbali ambayo yoyote anaweza kuwa nayo pindi anapotoa msamaha wake kwa mtu Fulani kulingana na uhusiano wake.

Kwa muonekano huo neno msamaha limepoteza radha yake na kwa namna hiyo imekuwa mtu kutoa msamaha wake kwa mwezake ila wa meamua kuishi maisha ya kisilani na mwezake.

Kuna watu wamekuwa wakisema moyoni mwao siwezi kumsamehe mtu huyu kwa vile alivyo nitendea ni makubwa na hayaelezeki.

Wengine wamethubutu kusema kuwa hata Mungu anaelewa kwa hili/lile jambo alilonitendea na hata nikisema ni msamehe mimi mwenyewe nitajishangaa sana na hata jamii inayo ni zunguka hatanielewa vizuri.

Na wengine husema ni kimsamehe kwa haraka hatasema mimi najipendekeza kwake au hatasema jambo hili alijaniumiza sana. 

imeandaliwa ;
                   
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                   
                     Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com
                                        
                                                  

                                                 Asante!!!!!!!!!!!!!!!!!!