Jumatano, 8 Januari 2014

TAMBUA MSAMAHA NA MAZINGIRA YAKE

MSAMAHA NA MAZINGIRA YAKE;


Kila kitu duniani ilikiende vizuri lazima pawepo na hali ambayo itasindikiza tendo/jambo hilo kutokea kwa ukamilifu wake, jambo ambalo alitasindikizwa na hali stahiki jua kitu hicho hakita kuwa na nguvu katika utendaji wake.

Kila kitu nguvu yake utegemea sana hali gani inayoisukuma jambo hilo litendeke pasipo hali hiyo jambo hilo linakuwa alina nguvu.

Tunapozungumzia hali ya kukufanya utende jambo tuna zungumzia shina ulilonalo katika utendaji wa jambo husika ambalo linakupa nguvu katika utendaji wake.

Mfano unapokuwa na furaha je, hali gani uliyonayo inayo sindikiza hicho kicheko kama hali inayokusindikiza katika kicheko sio sahihi basi hicho kicheko kinaweza kuitwa ni unafiki na hata unapolia je, haligani inasindikiza katika kilio chako napindi hali uliyo nayo ikatofautiana na hali uliyokuwa nayo basi uweza kuitwa ni unafiki.

Jambo lolote ili liwe imara utegemea sana shina la jambo hilo kwa hiyo uimara wa shina upelekea ubora wa jambo husika….kwakua uimara wa nyumba utegemea msingi wake na ubora wa mti utegemea sana mizizi yake.

Jambo lolote hili ulifanye katika ubora wake unahitaji sana ujue kwa ufasaha zaidi kwa nini nafanya jambo hili unapojua basi pajenga umaana wa wewe kufanya jambo hilo.

MSAMAHA limekuwa neno la kawaida katika jamii yetu inayotuzunguka, hakuna mtu hajawai kulitumia hili neno(katika maana ya kuambiwa au kusema) watu imefika wanachoka kusikia neno hili.

Hili neno limekuwa likitumika sana hatakufika mahali ambapo kushindwa nani ana maanisha na nani amaanishi imekuwa ikiwa katikati inaweza kumsamehe huyu kumbe huyu amefanya makusudi na unaweza usi msamehe huyu kumbe huyu akufanya kwa makusudi ki uhakika hili neno limekuwa liki wachanganya watu sana kwa watu wako njia ya panda hawajui wafanye nini bali wamekuwa wapweke kwa kutojua nifanye nini.

Kila mtu anakuwa na maamuzi yake pindi anapotaoa msamaha wake mwingine atasema nimekusamehe lakini usirudie tena,mwingine usema nimekusamehe lakini sitaki kukuona ukifanya jambo lilelile tena na kuwa na mtu Yuleyule tena,mwingine atasema nimekusamehe lakini sitaji tena kukuona katika maisha yangu tena, mwingine atasema nimekusamehe ila hama mahali hapa au mimi na wewe tutengane tusiwe pamoja tena na mwingine atasema nimekusamehe ila tufanye mapenzi mimi nawe ili tuyamalize kabisa au tumalize tofauti zilizopo kati yetu, au mwingine atasema nimekusamehe ila sasa utakuwa ukifanya hivi au utakuwa ukinifanyia hivi.

Haya yote ni mazingira mbalmbali ambayo yoyote anaweza kuwa nayo pindi anapotoa msamaha wake kwa mtu Fulani kulingana na uhusiano wake.

Kwa muonekano huo neno msamaha limepoteza radha yake na kwa namna hiyo imekuwa mtu kutoa msamaha wake kwa mwezake ila wa meamua kuishi maisha ya kisilani na mwezake.

Kuna watu wamekuwa wakisema moyoni mwao siwezi kumsamehe mtu huyu kwa vile alivyo nitendea ni makubwa na hayaelezeki.

Wengine wamethubutu kusema kuwa hata Mungu anaelewa kwa hili/lile jambo alilonitendea na hata nikisema ni msamehe mimi mwenyewe nitajishangaa sana na hata jamii inayo ni zunguka hatanielewa vizuri.

Na wengine husema ni kimsamehe kwa haraka hatasema mimi najipendekeza kwake au hatasema jambo hili alijaniumiza sana. 

imeandaliwa ;
                   
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                   
                     Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com
                                        
                                                  

                                                 Asante!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni