Jumatatu, 24 Februari 2014

MTU WA MAISHA YANGU



NAMJUAJE MTU ALIYE TAYARI KWA AJILI YA MAUSIANO YA KWELI,



Uwa watu hawataki kuhusiana tu bali kuusiana kuliko na mwelekeo wa manufaa na sio kuhusiana katika muonekano tu wa kuoneka tu mnausiana. Watu wengi wanapoingia kwenye mausiano katika akili njema( kuwa wangu katika maisha yangu siku zote ) uwa baada ya kujadiliana na uwezo wa akili yake katika kupambanua mambo au jambo hilo anapofikia hatma ya kukubali uwa anajua kwamba bila shaka huyu ni mwanaume au mwanamke wa ndoto yangu hivyo maisha yetu yatakuwa raha mstarehe lakini wakati mwingi imekuwa sivyo hivyo.

Kila mtu anaamua jambo kutokana na uwezo wa akili yake katika kupambanua jambo hilo lakini jambo hili uwa aliishii kwenye akili tu bali linagusa hata hisia za mtu tena katika hali kamilifu sana kuliko chochote na inawezekana kuwa ni kitu ambacho kinaongoza kukamata maisha ya watu wengi. Uwa ni matumaini ya watu wengi kuwa na mtu ambaye roho yake itampenda sana na kumwamini japo sio jambo rahisi kutambua kwani hiyo ni siri iliyo katika hazina ya moyo wake.  Nani kawaida mwanadamu kubadilika hivyo hatujui kuwa katika hali hii ya kubadilika je! Atabadilika katika hali njema au mbaya inategemea na muhusika mwenyewe kwakua dereva wa nafsi ya mtu ni mtu mwenyewe na sio mtu mwingine.

Limekuwa swali la watu wengi hasa walio kwisha tenda katika mausiano haya ya kimapenzi na hata wale ambao wako mbioni kuingia huko wamekuwa wakijiuliza maswali na kukosa majibu NI  NANI  ALIYETAYARI  KATIKA MAUSIANO YA KWELI  NAMI.Kwa hakika hakuna mahali utaenda nakupata majibu ya maswali haya ndivyo watu wengi wamekuwa wakifikiri. Na kwakua watu wengi wamekuwa na ndoto za kuwa na maisha ya wawili yaani ndoa hivyo jambo hili limekuwa ni changamoto kwa walio wengi na pindi wakiangalia mifano mibaya ya watu walio katika mausiano wapo watu wanauana, wanasalitiana, wanajeruhiana na wako watu ambao hawana furaha katika ndoa zao na wengi wao wamekuwa wakikaa kwa shindikizo la wazazi tu na wengine wanangojea watoto wakue aanze maisha mengine hii ni dalili mbaya na haina mvuto hasa kwa walio wengi wenye matarajio kuingia huko na wakati mwingine yeye mwenyewe anaweza kuwa mfano wa yale aliyopitia.

Lakini pamoja na hayo yote bado ningependa kusema kuwa ndoa ni kitu kizuri sana, ambacho akina mfano wake hapa duniani kwakua ndani ya ndoa kuna pumziko la kweli linalo kutosheleza lenye kuleta raha inayodumu, ni mahali ambapo moyo wako unapaweka nafasi ya kwanza hata kuliko jambo lolote. unaweza kuwa mahali popote ukapewa madini ya gharama kubwa lakini hapa linganishwi na raha iliyo ndani ya ndoa haielezeki na hata walio katika ndoa bado wanaona ni ajabu kwa ile amani na furaha ya kweli iliyopo na pia pamoja na hayo yote bado sio swala la kulikimbilia saaaana kwa wale ambao bado wanaona wanahitaji muda kwanza na kwa wale ambao hawajaruhusiwa kutokana na taratibu za jamii zao kwa ujumla wake.


Hapa kuna vitu viwili vya kuangalia kwa umakini mkubwa:

I.ALIYE TAYARI  KUINGIA  KWENYE  MAUSIANO

II.ALIYE TAYARI  KUINGIA   KATIKA   MAUSIANO  NA  WEWE

Ukiweza kuyajibu maswali haya kwa ufasaha basi ni wazi utakuwa umeshapata hatua moja ya msingi katika mausiano ya kimapenzi( ndoa).

I.ALIYETAYARI KUINGIA KWENYE MAUSIANO

Uwa swala la mapenzi alishurutushwi alipatikani kwa mabavu au kwa wazifsa wa mtu alionao kwa kuwa na wazifsa huo basi unasifa kumpata yeyote na kuwa huru kiasi kwamba kile unachotaka ndicho kinafanyika. Hautakiwi kwakua unakiu na kuwa na mpenzi basi hisia zako zinakuwa na nguvu katika maamuzi hata pasipo kuyapitisha katika chujio swala moja la kuangalia hapo ni UMRI si zungumzii tofauti kati ya wapenzi ambao waliokuwa zaidi ya miaka ishirini mathalani tofauti yao ikawa miaka mitano(5) au zaidi hapo mimi siingilii na utofauti haujalishi mwanaume mkubwa au mwanamke mkubwa bali inategemea makubaliano yao wahusika. Swala umri linakuwa na nguvu kwakua linahusiana uelewa ni kweli kwamba unapo mdogo uelewa wako unakuwa ni wakitoto tu hata ukipata uelewa mkubwa lakini hautajua usahihi wa kutendea huo uelewa na kitu kingine UELEWA wa mtu katika mausiano ya kimapenzi tambua naongelea mwenzi wa maisha na sio swala la kupenda kufanya ngono tu halafu ukahama hama kama nyumba ya kupanga bali ni maisha ya kujenga familia ya pamoja ila kabla ujatafakari uelewa wa mwenzako kuhusu mambo haya lazima kwanza wewe uwe na uelewa sahihi kwakuwa kipimo chako kitategemea na uelewa wako KUPENDA ni kitu kimoja na UELEWA ni kitu kingine kwakua hichi ndicho unabeba msingi wa mausiano yenu neno uelewa ni jambo muhimu sana na pindi usipolitilia mkazo wake stahiki ndipo utakapo tambua umuhimu wake baadae utakapo umekwisha chelewa sana. Katika kutafuta uelewa hapo hautakiwi umri japo mnaweza kuwa na umri unakubalika yaani zaidi ya miaka ishirini lakini kama uelewa ulibeba makusudi mema haupo basi ni vizuri uache kwa ustawi wa maisha yako ya baadae. Na kitu kingine YUKO TAYARI KIMAUSIANO lazima moyo wake uwe umefunguka kwa ridhaa ya mtu binafsi. Kwakua hili swala linahusisha hisia utayari wake wa kifikra utaweza kuruhusu hisia zianze kuwa hai, hili ni jambo la muhimu sana kwani mapenzi ni hiyari mtu katika kukuruhusu uwe mmoja kati ya wageni wake ndani ya moyo wake na hali hii mwanzo unaweza inaweza kuona ni dalili nzuri sana ila baadae ukaona tena utayari haipo tena usiyalazimishe na haya ni matokeo ya uelewa mliokua nao katika mausiano, hakikisha hakuna kilichomshurutisha mathalani wazazi,ndugu, au kile ulicho nacho. Ni vizuri akili itambue kuwa kuna kitu kinaitwa mapenzi na sasa nipotayari kuingia katika bahari hii ya wapendanao na utayari wao binafsi upelekea kila kuthamini na kujali hisia za mwenzake kwa moyo usio chembe ya uongo bali kweli tupu.

II.ALIYETARI KUINGIA KATIKA MAUSIANO NA WEWE.

Hapa ndipo tunasema kuwa huyu ndio chaguo langu la maisha yangu baada mchakato mwendo mzima wa ulimwengu, hapa hautuzungumzii kuwa mtu kuwa na UELEWA au YUKO TAYARI KATIKA MAUSIANO YA KIMAPENZI bali hatua hii sasa uthibitisho huyu ni wangu na wala si wa wengi. Hatua ndio inapelekea watu kufa, majeraha na mambo mengine mabaya yanazaliwa hapo kwakua kunamategemeo waliokuwa nayo na matarajio ya maisha bora ya maisha bora ya hapo baadae.

Nawezaje kumtambua sasa!!!!!!!!!!!!

(a)anakuzungumziaje?

Kama kweli kitu kimemla moyo wake uwasahau kukuzungumzia sio mkiwa wote bali hata mkiwa hampo wote bado atakuwa kero kwa wenzake hata itawafanya marafiki watafute kukujua huyu ndio nani? Mara nyingi inakuwa uthibitisho katika kupigia simu mara nyingi na meseji zi sizo koma na pasipo kujua ni wakati wagani usiku mchana au usiku au unafanya kazi gani anachojali ni kufurahisha hisia zake juu yako na hali hii inawakumba watu wote sio upande mmoja kila mtu anakuwa anakiu na mwenzake. Japo mnapoanza si vile mtavyokuwa mkiendelea, utofauti unaweza kuwa na nguvu na kupunguza hile kasi yenu na kuanza kulaumiana sana kwa huo utufauti hua unausishwa na uelewa usio sahihi kuhusu hayo mausiano.

(b)lazima ajione yeye ndio wewe

Sio ile kwenye meseji tu ni hali inayoishi kuonekana pasipo kuko a yenye kudhihirika hata katika kutoa zawadi mmoja na mwenzake. Lazima iweakiona unafuraha kwakile alichokifanya hicho ndicho kicheko chake na hata furaha yake.
Lazima aone kuwa thamani yake sio bora kama thamani yako kwake na hivyo wote mjione hivyo kwakua kila mtu ana muona mwenzake ndio furaha ya siku yake ila isiwe sinema uwe ni moyo unaongea na huku ukijua kile unachokiongea kwa akili timamu tena katika hali ya kupenda.

(c)mapenzi yenye kumuhusisha Mungu

Mapenzi ameyanzisha pale edeni alipomtengeneza eva kwa ajili ya ajili ya adamu, yeye ndio fundi sahihi wa kuboresha mapenzi na kuleta chachu lakini huu utundu wa sasa katika ulimwengu tulio nao sasa ndio matokeo kuvunjika saaaana katika mausiano ya kimapenzi tambua kesho yenu hamuijui basi mapenzi yenu ya mtambue Mungu kwa udhati ili yeye alete Baraka na furaha katika maisha yenu tangu sasa hadi milele AMINA.

Imeandaliwa na;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com

                              “BARIKIWA ………SANA”