Jumanne, 3 Septemba 2013

MWANZO MPYA



MWANZO MPYA


New beginning…………………..!!!!

Pindi unapokosea jambo fulani ni vizuri uanze mwanzo kuliko kuhisi ulipokosea halafu ukakosea zaidi anza upya utajua wapi umekosea na nifanyeje.


Mwanzo mpya au ukurasa mpya wa mtu katika kuanza upya maisha yake ni jambo lenye sura mbalimbali wapo watu wataona ugumu,wengine wataona kuchekwa na wengine wataona ni kupoteza muda na hata wengine hawataona thamani ya kuanza upya.

Mathalani nyumba unapoikalabati ni tofauti na mtu anaye amua kuanza upya katika ujenzi japo ni kweli kuna gharama kubwa sana mtu ambaye ataamua kujenga upya tofauti na mtu yule ambaye ameamua kukalabati maana yule ambaye aliye amuakujenga upya atakuwa amejihakikishia uimara zaidi kuliko yule aliye amua kukalabati.

Hata katika gari lililo karabatiwa sana na yule aliye amua kununua gari jipya lipi ni suluhisho la kudumu ambalo litakusaidia kwa muda mrefu.

Wakati mwingi tumekuwa tukitafauta unafuu katika mambo yanayo tukabili na sio kuliondoa tatizo kwa ujumla wake,na ni wazi ukitafuta suluhu ya muda ndiyo utayoipata ambalo baadae jeraha litaibuka tena. Hii hiko wazi hatuwezi kuwa salama kwa sisi kutafuta unafuu kwa kuwa unafuu ni akiba ya baadae au ni mlipuko ambao unaweza lipuka wakati popotena kwa mtu yeyote..
Marko 11:15-16

Hata katika biblia tunamuona yesu akisema;
“nitaliboa hekalu hili na kulijenga siku tatu…..”


Kwanini yesu akusema nililekebishe hili hekalu kwa kuwa katika kulekebisha kuna uimara mdogo lakini katika kujenga upya kuna uimara unaodumu milele.


Moyo uliojeruhiwa dawa ya pekee ni kuanza upya kabisa!!!!!!
Tatizo kubwa watu wanapo umizwa moyo au kujeruhiwa mioyo basi wanatumia ujanja na kasi katika kutaka kuziba nafasi zilizo kuwa wazi!

Uwa hawatumii muda wao katika kutafakari kwanini haya yametokea na mimi nijipange kwanamna gani ili yale yasifanane na haya, na hali hii mara nyingi upelekea kuumizwa zaidi na kujeruhiwa na kusababisha hatimae kujenga majenzi ambayo ni vigumu kuyaondoa kwani hayaondolewi kila hisi.

Mtu alijeruhiwa moyo kwa kukosa kujua nini cha kufanya upelekea kufanya lolote ambalo litakuja kichwani mwake utegemea na uelewa wake kuhusu hayo mausiano haya wapo watu wanathubutu kusema sitamwamini mwanadamu tena,hata wengine upelekea kujiua…..!

Kama mtoto anzapo hatua ya kutembea kuna kuanguka lakini mwishoe usimama lakini katika mausiano yanapo vunjika ili uendelee vizuri ni vizuri uanze upya katika ubora ulio mzuri zaidi na sio kukulupuka.


Namna ya kuanza upya kwa mtu aliye na moyo uliojeruhiwa!

I.ikubali hali iliyotokea na wewe ndio muathirika wa jambo hilo.
Tunapozungumzia kukubaliana na hali iliyopo hatuna maana kuwa ni jambo mbalo umelisababisha wewe  la! Asha bali ni jambo ambalo limegusa moyo wako limeleta matokeo ambayo yameathiri maisha kwa namna moja au nyingine.

Hali hiyo uone sasa tatizo limesha kupata ona Mungu anatambua majeraha ndani yako na anategemea jambo ambalo jipya lenye utukufu wake kuzaliwa ndani yako.

Usitumie wakati wako kumlahumu mtu kwani hata ukimlahumu mtu haita saidia kitu tambua wewe ndio muhusika na maisha yako kupitia wewe unaweza kutengeneza kesho iliyo bora kama ulivyoitengeneza ikawa leo kwa vile ulivyo kuwa jana.

Lazima utambue wote wanaweza kufarahia watakapo kuona uko vizuri na wala si wakuone vibaya lakini ni Mungu tu anayeweza kukutengeneza vile tu utakiwavyo kuwa.

Watu wanaweza jua uko kwenye tatizo lakini namna ya kutoka hapo kunaweza kuwa shida wakati mwingine baada ya kutoka wanaweza kuongeza jambo likawa ni tatizo kubwa.


II.kubali kuwa huo ndio muonekano wa maisha yako ya nyuma.

Tambua kuwa hakuna mtu asiye historia yake na kuna uwezekano wa kuwa tofauti hivyo kubali kuwa hiyo basi ni historian a wala sio jambo jingine.

Hakikisha nyuma isikusumbue bali mawazo yako ya mbele ya chukue nafasi na kupanga mikakati ya namna ya kuboresha kesho.(kitu ambacho kikusumbue katika kichwa chako namna nawezaje ni kufanya kesho yangu ikawa tofauti na leo na huku ukiona uwezo wa kufanya jambo upo pasipo na shaka yoyote kwakua una mwamini Mungu yeye asishindwa).

Hakikisha usiishi maisha ya unyonge kwa kuwa huruma ya kibinadam haina hatma njema katika maisha yako binafsi.( binadam wote wanahitaji faraja maisha yao yote hakuna siku hatatosheka)
Ni wewe unaweza fanya jambo likapita au jambo likadumu ndani ya maisha yako kwa kulipa nafasi.
Jua kwamba hiyo ni histori ya maisha ambayo ni tofauti na mwingine hivyo jua inahitaji ibaki kama kumbukumbu lakini isiwe dira ya maisha yako au ikazalisha maisha ya uwoga katika kuchukua maamuzi mazuri katika maisha yako.

Ni lazima mtu ili awe wa maana sio lazima alikuwa wa maana toka awali bali wapo walikuwa hawana historia ya kuvutia na mwisho wake ulikuwa ni ushuhuda mzuri.


III.utambue mtazamo wa Mungu juu yako.

Unapo muona Mungu ni zaidi ya baba,mpenzi,rafiki hivyo ndivyo alivyo hama kwa hakika hakuna mfano wako na wala hatatokea.
Biblia inasema;
-sikuja kwa ajili ya wenye haki bali wenye dhambi ili wapate kutubu.

Na vilevile inasema tulipokuwa wenye dhambi Mungu alitupenda zaidi, huna haja ya kuona wanadam wanavyo kuona basi ndivyo Mungu anavyo kuona.

Na Mungu sifa kubwa anaangalia mwisho wenye ushuhuda huwa angalii ulianzaje bali anangalia umemalizaje na sio jambo jingine, mathalani katika riadha mshindi anatambuliwa mwanzo wa mbio au mwisho wa mbio.
Huna haja ya kukata tama bali zidi jua hata kama mwili wangu najiona sifai  kuwa mme/mke jua bado unafaa sana kwa Mungu nae anaweza kukutengeneza ukawa bora hata kuliko mwanzo.

Kama ni msomaji wa biblia mzuri basi utamtambua AYUBU jinsi kesho yake ilivyokuwa ya kutamanika kuliko jana yake.
                         Yakobo 5:11
Ni vizuri kutambua kuwa anaweza kubadilisha kesho ikawa nzuri  kuliko ni wewe na Mungu na wala si mtu mwingine.

Prepared by ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com


“TUNAKUTAKIA MWANZO MZURI”
We wish you good beginning………….

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni