Jumamosi, 3 Agosti 2013

KUWA MTUMISHI WA MUNGU

                                        KUWA MTUMISHI WA MUNGU
Kumtumikia Mungu Kama apendavyo:
Ni jambo ambalo Mungu analitarajia litokee kwa mtu ambaye amemkubali kuwa yeye ni Mungu wake.
Waefeso 4:1-4

Wafilipi 1:27-29
Kwa hakika maisha ya ushindi mwelekeo sahihi wa kiMungu unakuja kwa usahihi ni pale tu utakapojua maana ya kumtumikia Mungu, na hii ni kawaida ya Miungu yote haiwezi kukufanikisha mpaka pale umeitumikia kwa namna inavyotaka yenyewe yani umewafanyia ibada ambayo wamekubali.
Wakolosai 2:6
Hili neno la kawaaida masikioni mwa watu wengi lakini kulisikia peke yake pasipo kueleweshwa na Mungu mwaenyewe ni ngumu kulielewa kwa namna yake.
Ukitaka kuupendeza moyo wa Mungu lazima ufikirie namna ya kufanya kitu mbele zake naye afurahie uwepo wako duniani.(hiki ndicho Mungu anakitaka kwako maadam ukishakielewa hiki hakuna kushindwa)
Na namna unavyomtumikia Mungu hicho ndicho kipimo sahihi namna unavyo mpenda.(kutumika kwa kupenda ni vizuri kwakua ni ishara ya kujua wajibu wako)
Kama kunakitu kikusumbue au kukinyime raha ni kutafuta namna ya kumtumikia Mungu kwa usahihi wake pasipo kushurutishwa wala kulazimishwa maana hapo ndipo palipo na ustawi wa maisha yako yaani chemchem isiyokauka, raha yako itokane baada ya wewe kutambua maana ya kumtumikia Mungu kuanza kumtukia Mungu.
Wafilipi 3:12
Sura ya Mungu,tabia zake,uwezo wake utaona kwa ukamilifu pindi utakapo kuwa ndani ya utumishi wake.
Kitu cha maana kwa Mungu ni wewe kuandaa mazingira ambayo Mungu atatenda kazi pamoja na wewe kwa namna yake.
Kama ukishindwa kutafuta na kujibidisha namna ya kumtumikia Mungu  sahau kuona mtembeo wa ki Mungu ndani ya maisha yako na una haja kujivunia katika wokovu.
Iwathesalonike 1:8-9
Hii ni siri pekee ya kukaa na miungu yoyote duniani ni kuitumikia na hakuna jambo linguine.
Nje  ya utumishi wa kweli mambo yote unayofanya hayana kibali kwa Mungu yaani kutoa,kuomba,kuimba n.k
Na maisha haya ndiyo yanakupa nguvu kusema mimi ni mali ya kristo kwa kuwa unamtukia yeye naye anayafurahia muungamaniko wenu.
Kumtumikia Mungu sio shida si kwasababu unaogopa jehanamu labda kuna urafiki kufanya jambo Kwa shirika lakini sio kumtumikia Mungu Kama apendavyo yaani una mtumikia Mungu Kama alivyo hakuna usaidizi mwingine.
.utendaji wa yesu ulitegemea Mungu anasemaje?
                                                     Yohana 8:29                         
Hakuna kitu kigumu kama kumtumikia Mungu katika matakwa yake yaani kufanya jambo kwa namna yake (vile awazavyo katika akili yake Mungu)
                                                        Luka 14:25-35, 17:33
                         
 I.hakuna kutoa hakuna kupata (no give no gain)               
 Japo hatutoi ili kupata bali ni kutekeleza maagano yetu kwake, ishara ya kuzingatia makubaliano yako na Mungu.
Maisha ni shamba japo si namna ya mwili bali katika roho, kama hauta toa hakiwezi kupata
-shamba lina sifa kubwa kupanda na kuvunwa, hivyo kama hakuna kupanda hakuna kuvuna hii ipo halisi sana.
Kutoa ni ishara kubwa sana kuwa Mungu anahusika na maisha yako hivyo unahusika na mambo yake kwa kutoa KWA AJILI YAKE.
Hili limekuwa jambo la adimu kwa watu wanaoenda kanisani kwa sababu ya kutembea mwilini au kutoa maslai binafsi kwanza.
Watu wengi hawaendi mbele kwa sababu hawajajua misingi halisi ya kutoa,wanatoa pasipo ukamilisho.
Lazima ujifunze kutoa fedha,muda,nguvu yako katika kuimarisha mwingiliano wako na Mungu. Utoaji wako mbele za Mungu hiyo ni ishara kubwa ya kumtegemea Mungu
Utoaji uliokamili inamaana kuwa moyo wako uko wazi kwa Mungu naye Mungu aweze kukupa kibali katika maisha yako.
Unapo penda kutoa muda wako,fedha na vitu vingine havina shida nabado unaona haitoshi sikuzote utafikiri namna ya kutoa zaidi ili akufurahie.
Usipotoa mwili wako kwa ajili Mungu tambua utatumika kwa ajili ya mambo mengine,magonjwa,mawazo yasiyo kuwa na maamuzi/yasiyo na muafaka wa kudumu na mambo mengi yatapata nafasi ndani yako.(ndoto za kubomoa ufalme wa Mungu ndani yako,uvivu katika mambo ya Mungu)
Hii ni ishara ya kujipima kwa Mungu ni namna gani unamjua,unamwitaji,thamni yako kwake hauhitaji kuweka mjadala kujitambua.
Kwakua Mungu alionyesha kukupenda pale tu alipotoa pumzi yake,uzima wake na hata mwanae wa pekee,kwaiyo utoaji ni msingi mzuri kuonyesha upendo.
                                                  Yohana 3:16
Kuwa na kitu wakati unae mpenda anakiitaji yupo hiyo si ishara ya kupenda hata kidogo(unayo nguvu,fedha n.k) huo ni unafiki wa kiwango cha mbele za Mungu,haimfurahishi Mungu na muda si mrefu utaona matunda ya kutomfurahisha Mungu(huwezi kutoka hatua moja kwenda nyingine kiafya,kiuchumi).
Usipojitoa usitegemee yeye kujitoa kwako.
                                               Wagalatia 6:7
 Prepared by,
                    Cothey Nelson  - 0764 018 535
                                                cotheyn@yahoo.com
                     
                      James katiti      -  0713 398 042
                                                james.adili19@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni