Kumtumikia
Mungu Kama apendavyo:
Ni
jambo ambalo Mungu analitarajia litokee kwa mtu ambaye amemkubali kuwa yeye ni
Mungu wake.
Waefeso
4:1-4
Wafilipi
1:27-29
Kwa
hakika maisha ya ushindi mwelekeo sahihi wa kiMungu unakuja kwa usahihi ni pale
tu utakapojua maana ya kumtumikia Mungu, na hii ni kawaida ya Miungu yote
haiwezi kukufanikisha mpaka pale umeitumikia kwa namna inavyotaka yenyewe yani
umewafanyia ibada ambayo wamekubali.
Wakolosai
2:6
Hili
neno la kawaaida masikioni mwa watu wengi lakini kulisikia peke yake pasipo
kueleweshwa na Mungu mwaenyewe ni ngumu kulielewa kwa namna yake.
Ukitaka
kuupendeza moyo wa Mungu lazima ufikirie namna ya kufanya kitu mbele zake naye
afurahie uwepo wako duniani.(hiki ndicho Mungu anakitaka kwako maadam
ukishakielewa hiki hakuna kushindwa)
Na
namna unavyomtumikia Mungu hicho ndicho kipimo sahihi namna unavyo
mpenda.(kutumika kwa kupenda ni vizuri kwakua ni ishara ya kujua wajibu wako)
Kama
kunakitu kikusumbue au kukinyime raha ni kutafuta namna ya kumtumikia Mungu kwa
usahihi wake pasipo kushurutishwa wala kulazimishwa maana hapo ndipo palipo na
ustawi wa maisha yako yaani chemchem isiyokauka, raha yako itokane baada ya
wewe kutambua maana ya kumtumikia Mungu kuanza kumtukia Mungu.
Wafilipi
3:12
Sura
ya Mungu,tabia zake,uwezo wake utaona kwa ukamilifu pindi utakapo kuwa ndani ya
utumishi wake.
Kitu
cha maana kwa Mungu ni wewe kuandaa mazingira ambayo Mungu atatenda kazi pamoja
na wewe kwa namna yake.
Kama
ukishindwa kutafuta na kujibidisha namna ya kumtumikia Mungu sahau kuona mtembeo wa ki Mungu ndani ya
maisha yako na una haja kujivunia katika wokovu.
Iwathesalonike
1:8-9
Hii
ni siri pekee ya kukaa na miungu yoyote duniani ni kuitumikia na hakuna jambo
linguine.
Nje ya utumishi wa kweli mambo yote unayofanya hayana
kibali kwa Mungu yaani kutoa,kuomba,kuimba n.k
Na
maisha haya ndiyo yanakupa nguvu kusema mimi ni mali ya kristo kwa kuwa
unamtukia yeye naye anayafurahia muungamaniko wenu.
Kumtumikia
Mungu sio shida si kwasababu unaogopa jehanamu labda kuna urafiki kufanya jambo
Kwa shirika lakini sio kumtumikia Mungu Kama apendavyo yaani una mtumikia Mungu
Kama alivyo hakuna usaidizi mwingine.
.utendaji
wa yesu ulitegemea Mungu anasemaje?
Yohana
8:29
Hakuna
kitu kigumu kama kumtumikia Mungu katika matakwa yake yaani kufanya jambo kwa
namna yake (vile awazavyo katika akili yake Mungu)
I.hakuna kutoa hakuna kupata (no give no gain)
Japo
hatutoi ili kupata bali ni kutekeleza maagano yetu kwake, ishara ya kuzingatia
makubaliano yako na Mungu.
Maisha
ni shamba japo si namna ya mwili bali katika roho, kama hauta toa hakiwezi
kupata
-shamba
lina sifa kubwa kupanda na kuvunwa, hivyo kama hakuna kupanda hakuna kuvuna hii
ipo halisi sana.
Kutoa
ni ishara kubwa sana kuwa Mungu anahusika na maisha yako hivyo unahusika na
mambo yake kwa kutoa KWA AJILI YAKE.
Hili
limekuwa jambo la adimu kwa watu wanaoenda kanisani kwa sababu ya kutembea
mwilini au kutoa maslai binafsi kwanza.
Watu
wengi hawaendi mbele kwa sababu hawajajua misingi halisi ya kutoa,wanatoa
pasipo ukamilisho.
Lazima
ujifunze kutoa fedha,muda,nguvu yako katika kuimarisha mwingiliano wako na
Mungu. Utoaji wako mbele za Mungu hiyo ni ishara kubwa ya kumtegemea Mungu
Utoaji
uliokamili inamaana kuwa moyo wako uko wazi kwa Mungu naye Mungu aweze kukupa
kibali katika maisha yako.
Unapo
penda kutoa muda wako,fedha na vitu vingine havina shida nabado unaona haitoshi
sikuzote utafikiri namna ya kutoa zaidi ili akufurahie.
Usipotoa
mwili wako kwa ajili Mungu tambua utatumika kwa ajili ya mambo
mengine,magonjwa,mawazo yasiyo kuwa na maamuzi/yasiyo na muafaka wa kudumu na
mambo mengi yatapata nafasi ndani yako.(ndoto za kubomoa ufalme wa Mungu ndani
yako,uvivu katika mambo ya Mungu)
Hii
ni ishara ya kujipima kwa Mungu ni namna gani unamjua,unamwitaji,thamni yako
kwake hauhitaji kuweka mjadala kujitambua.
Kwakua
Mungu alionyesha kukupenda pale tu alipotoa pumzi yake,uzima wake na hata
mwanae wa pekee,kwaiyo utoaji ni msingi mzuri kuonyesha upendo.
Yohana 3:16
Kuwa
na kitu wakati unae mpenda anakiitaji yupo hiyo si ishara ya kupenda hata
kidogo(unayo nguvu,fedha n.k) huo ni unafiki wa kiwango cha mbele za
Mungu,haimfurahishi Mungu na muda si mrefu utaona matunda ya kutomfurahisha
Mungu(huwezi kutoka hatua moja kwenda nyingine kiafya,kiuchumi).
Usipojitoa
usitegemee yeye kujitoa kwako.
Wagalatia 6:7
Prepared by,
Cothey Nelson - 0764 018 535
cotheyn@yahoo.com
James katiti - 0713 398 042
james.adili19@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni