Alhamisi, 22 Agosti 2013

RAFIKI NI NANI?



RAFIKI NI NANI?

Rafiki ni mtu wa muhimu sana,kwakua katika kuwa nae unapata kujua upande mwingine wa maisha yaani nini  huyu rafiki yako amepitia katika mwenendo mzima wa maisha yake na nini anajua kuhusu maisha kwa ujumla wake(mtazamo wake kuhusu maisha) kwakua pasipo yeye kukutana na wewe usinge ya jua, vilevile katika kukutana/kuwa na rafiki unaweza kubadili kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine(mchango wake katika kuyainua maisha yako kimawazo au uchumi)
Ni kawaida rafiki mzuri watu hudumu nae nautamani kuishi nae wakati wote na rafiki asiye mzuri watu uvunja husiano wao,kwakua hukosa kuona umaana wa kuwa na rafiki pasipo kuona mchango mzuri  katika maisha yake.

Hivi ni rahisi kutambua huyu ni rafiki mzuri au rafiki mbaya kwakusikia habari zake au kwa kumuona kwa kipindi kifupi?
Rafiki ni mtu muhimu sana kwakua wako watu  waliotoka kimaisha kutokana na msaada wa rafiki na wako watu ambao hawajatoka kimaisha kutokana kutokana kukosa rafiki au kukosa rafiki ambaye anayeweza kumtoa mahali alipo na kwenda sehemu nzuri.
Sikuzote matarajio ya rafiki ni kuwa nae wakati wote akusitiri katika aibu yako na akukosoe katika pale unapoenda vibaya na rafiki wa namna hii ndipo utaona umaana wa kujivunia urafiki wenu,
Ninapozungumzia rafiki inawezekana kuwa wa jinsia yoyote wa kike au wakiume ili mradi anatimiza wajibu wake kama rafiki.(rafiki ni rafiki jinsia sio jambo la kulipa kipaumbele kwa kuwa alina maana unachohitaji ni kupata mtu ambaye anatambua nafasi yake kwako.
Katika dunia tuliyonayo wako watu ambao wameinuka kutoka na usaidizi rafiki walio karibu sio nyanja moja bali sehemu yote ya maisha binafsi.
                                                               Rafiki wa karibu!
Mtu naweza kuwa na rafiki aliye mbali na aliye karibu (mtu ambaye mnaonana mara kwa mara) na kushirikiana katika mambo mnayo yakabili pamoja.
Mtu ambaye athri yake inawezekana kuonekana kwa haraka ni Yule aliye karibu yako kwakua jambo atakalofanya litakuwa udhihirisho mkubwa.
Lakini kumbuka kuwa sio wote unao wapenda wanafaa kuwa marafiki zako, kwakua kunatofauti kubwa kati ya watu unao wafahamu na watu ambao ni marafiki zako. Japo wote unaweza kuwashirikisha lakini yako kuna kitu unategemea akifanye ili arudishe matumaini ndani ya moyo wako.
Vile rafiki yako alivyo ndivyo atakavyo weka namna yako utakavyo onekana endapo tu kama utamkubali ndani ya maisha yako, kwakua unaweza kuwa na mtu aliye karibu sana na wewe na hata mkashirikiana mambo mbalimbali hata ya mwilini lakini usimpe nafasi ndani yako na wala asi athiri maisha yako.
Iwakorintho 15:33
Ni hatari sana kuwa narafiki ambaye hakusaidii kukupeleka katika njia ambayo Mungu anataka uende.(udhihirisho wa urafiki wa kweli haupo katika kusema tu bali ni mchango unao onekana ndani ya maisha yako)
II nyakati 22:4-5
Mathayo 16:26
Rafiki asiye jua apasalo kufanya kwako huyo ni sumu sana kwakua kwakua anaweza kukupeleka kusiko kusaidia lakini kwa rafiki anayetambua wajibu wake kwako yeye anaye weza kurudisha furaha mahali pasipo na furaha na matumaini pasipo matumaini, kicheko pasipo kicheko na hata kuondoa upweke na simanzi ndani yako.
Ni wazi rafiki mzuri ili afanye mazuri juu yako kwanza hauna budi kumtambua halafu ukampa nafasi, pindi unapokosa kumtambua halafu ukampa nafasi ndani yako anaweza fanya jambo ambalo litaweka historia katika maisha yako.
Ili mwende pamoja lazima muwe zaidi ya kuwa pamoja yaani muwe na nia moja katika kukubaliana yale mtakayofanya katika moyo ulio safi.
Kamwe rafiki yeyote ambaye amjaambatana katika kunia mamoja ni vizuri kuachana nae kwakua uwezi kumsaidia kwa kumvumilia/kwa kuvuta subira atakuharibia au kukuchelewesha.
Lazima upate rafiki ambaye mtazungumza mambo ambayo yatapata kibali kwa Mungu katika maendeleo yenu binafsi na hatma njema iliyojaa Mungu mbali na hapo utapotea hakuna mapumziko.
Mithali 14:12

                                           Sifa za rafiki aliye bora:
Kumbuka kila rafiki ambaye unae anao mchango katika kukutengeneza au kukuharibu jambo hili lazima ulichukulie katika uzito wake.
Maandiko ya mungu yanasema,
“ndege wanaofanana ndio wanao ruka pamoja….”
Asikudanye mtu siku zote kile unacho kisikia, kukiona na kikipata nafasi ndani yako kinafanyika sehemu ndani ya maisha yako.
Kama unataka kuwa mtu wa maana lazima uwe na rafiki ambae ni wa maana vile rafiki yako alivyo ndivyo atakavyotoa mchango wake.

                                            I .awe anamjua Mungu.
Tambua kile alichonacho rafiki yako ndicho atachokupa sio kitu kingine ambacho hana, ni vizuri maisha yaonyeshe kweli anamuhofu Mungu,
Sio rafiki kila jambo yeye ni shabiki tu ajali jambo hili lina mpendeza Mungu au la! yeye ukulupikia maadam lina manufaa kwake.
Tambua sisi sote tumetoka kwa Mungu na kwa Mungu tutarudi, mambo ya dunia yanapita japo yanavutia ila angalia yasikutenge na Mungu kwakua Mungu yupo mahali pote na hata dumu milele.
Hivyo rafiki mzuri pamoja na mambo mengi ni mtu anayekukumbusha kuwa umetoka wapi?
“Watu wawili hawawezi kwenda pamoja isipokuwa wamepatana”
Hakikisha mwenendo mnatembea ni mwendo ulio na nuru ya Mungu ili mambo yenu Mungu hayafanikishe.

                                                II.anayejiheshim
Ni vizuri huyo rafiki lazima ajue maana ya heshima na anayejiheshim na anawaheshim watu wengine.
Tunapozungumzia hatuzungumzii ustahara wa kusalim (kupiga goti, sauti ya upole) ni zaidi hapo heshima ni namna unavyowaelewa watu na utu wao.
Anachokifanya ndicho hicho anachokimaanisha hana utofauti wa kauli ya mdomo na moyo wake.
Thamani ya watu kwake huwa haijengwi na kipato cha fedha, muonekano au maneno mazuri ambayo yanazungumzwa na mtu husika.
Ni mtu ambaye anawajali watu Kama anavyo mjali Mungu kwa kuwa watu tumetoka kwa Mungu kumpenda Mungu pasipo kuwapenda watu ni bure.
Luka 2:52
Japo wanadamu wote sio wema bali wewe fanya wema kasha uende usingoje matokeo.
Maandiko yanasema:
“Utampendaje Mungu usiye muona wakati unamchukua jirani yako……”
Katika dunia ni jambo la kawaida kumchukua binadamu wenzako halafu ukasema nampenda Mungu.(huwezi kuwapenda wazazi halafu ukawachukia watoto kwakua watoto ni sehemu ya wazazi)
Mathayo 5:43-48


                                                 III.kielelezo safi
Rafiki mzuri lazima mwenendo wake unakuwa mwelekeo mzuri na sio lazima awe kiongozi wa jamii,japo anaweza kuwa kiongozi wake binafsi.
Ni mtu ambaye anajua iko jamii wanahitaji kujifunza kupitia yeye inategemea na rika alilonalo
Kielelezo safi ni kitu muhimu sana kwakua atakuachia mambo ya mazuri ambayo utayatumia kaika maisha yako.
Ni kweli unaweza kuwa na watu wengi wasiwe kielelezo kwako lakini asiwe rafiki kwakua ana nguvu ya kukushusha au kukuimarisha.
Lazima kielezo safi ziwe sifa ambazo binafsi anazizingatia kwa mwenendo mzima wa maisha yake binafsi.
Mathayo 5:16
Japo kuna watu wenye maadili mema lakini pamoja na hayo unahitaji kuwa na Mungu ili akuwezeshe kudumu katika kielelezo safi kwani katika dunia ya sasa unaweza kukutana jamii wakabadilisha ule mfumo wako wa maisha kwa ujumla wake.
Hakikisha awe anaongea mambo ambayo yanajenga yaliyo na mufaa kwa jamii inayo mzunguka, sio mtu aliye jaa majungu na visasi ndani yake,
                                                    IV.mwazi,mkweli
Lazima anapokuwa na wewe ni mahali ambapo moyo wake unakuwa na nguvu na kusonga mbele kwa hali hiyo ni lazima awe mwazi kwako( hali ya kweli itoke ndani yake aseme kanakwamba anajiambia mwenyewe)
Hii ni moja ya nguzo ya kweli katika maisha  yenu kama hamna hali hii jua kwamba urafiki wenu unauhalakini au dosari au kutoaminiana.
Lazima muonane ninyi ni zaidi ya kila kitu pindi mnapo kutana mnajenga vitu ambavyo vinakuwa na faida katika maisha yenu binafsi.
Kama rafiki ambaye sio muanzi jua huo urafiki wenu unadosari kuwa makini au jipange kwa lolote kutokea wakati wowote.
Uwazi ni ishara kubwa sasa mmeanza kuingiliana katika urafiki wenu katika usahihi pasipo unafiki.(uwazi ni kama kuwa uchi kwa huyo rafiki)
Japo ni mtihani mkubwa kutambua ukweli kuhusu mambo anayokwambia hivyo usiwe mwepesi wa kuamini mpaka pale moyo utakapo jiridhisha.

                                                  V.anayekubaliane kuonyana
Kila mtu awe na uhuru wa kumuonya mwezake kwa upendo, na kila mtu awe tayari kumsikiliza mwenzake kwa kile  anacho mwambia.
Pamoja na hayo usiwe mwepesi katika kuchukua maamuzi jaribu kutulia na kwa upendo ulio nao na rafiki unaweza kitu kilicho bora zaidi ambacho kitafanya urafiki ukawa wa maana sana.
Katika tofauti zenu na namna mnavyo zimaliza hapo panaudhihirisho wa ubora wa urafiki na kumaanisha kwenu.
Hasitokee mtu ajione mwenye haki kuliko mwezake kwakua wote mnakamilishana katika kuleta maendeleo yenu.
Msikilizane namuonane kuwa wote mnahitajiana katika kutegemeana kwa ajili ya kufanikisha yaliyo mbele yenu.
Hapa ni sehemu  muhimu sana kwakua inaonyesha kwa kiasi mnaingiliana katika kutimiza lengo lenu, hii hatua isipo fanyika kwa ungalifu inaweza leta madhara makubwa sana.
Hii hatua inakuwa na shida sana kama tu hamjatambua misingi ya urafiki wenu na kuipa nafasi kwa ajili ya kufikia mahali mlipo kusudia.
Mnapokuwa mkisaidiana jua kwamba hakuna mtu ambaye alikuwa vizuri kwa asili yake bali wote wanatengenezwa kuwa vizuri wanao kubali basi wanakuwa vizuri.
Mashindano sio sehemu yenu,japo kutakuwa na mpishano ila msiluhusu katika mabishano yenu yaendelee huku mkiwa katika mausiano ya urafiki.

                                                VI.mpenda maendeleo ya pamoja.
Rafiki mzuri lazima athamini maendeleo yako na hauzunike katika matatizo ya wengi hii ni shida sana kwa marafiki walio wengi katika kutekeleza swala zima.
Pindi utakapo muona mtu anaelewa vizuri swala linalo kukabili halafu akawa na wewe kanakwamba aelewi kinacho kukabili huyo si rafiki mzuri.
Kama kweli ni rafiki mzuri huwa atapenda kuona furaha yake basi panakuwa na furaha yako ili wote mfurahi pamoja.
Hakuna urafiki ulio mzuri kama ukimuona mwenzako analia nawe ukalia pamoja nae ili siku nawe utakapolia mlie wote.
Ni mtu katika mipango yake mizuri uwa anakufikiria na wewe pia anakuhusisha pale inapo bidi.
Ni mtu anayejali kesho yako iwe katika hali iliyo njema na usahihi ili kuleta katika ustawi ulio bora nakufanikisha yale yaliyo magumu kwake.
Hali hii pia iwe ndani yako na wala usiitegemee kuiona kwa mtu mwingine wakati wewe ndani kuna ubinafsi kamwe kudumu katika huo utofauti wa namna hiyo.
Hii ni ishara kubwa sana ya kutambua udhati wa urafiki wenu nikutambua nafasi yako kwake vile anavyokutambua ndivyo atakuhusisha inje ya hapo hawezi kukuhusisha.
Uwezi kujivunia huyu ni rafiki mzuri kama tu ujaona kwa udhati namna anavyo husika na maisha yako kujua unafanya nini sasa na unamatarajio gani na je! Utafikaje huko.
Urafiki sio kula pamoja wala kulala pamoja, au kushirikiana katika nguo bali namna gani unavyomuandalia/mfikiria kesho nzuri ndugu yako.
Japo unatakiwa kuwaza vizuri kwa wote lakini rafiki lazima usimamie kuhakikisha kuahakikisha mnaenda pamoja.
Ifike kipindi mtu mmoja akipata na mwingine akikosa haina shida kwakua unajua akipata yeye basi umepata wewe kama sivyo basi huo sio urafiki wa kweli.
                       
                                          VII.anayetambua/thamini udhaifu wako,
Rafiki wa kweli huwa atumii udhaifu wako katika kukufanya uwe mnyonge bali usimama katika nafasi ya kukutegemeza ili uweze kuimarika na uonekane wa maana sana.
Tambua unapotambua udhaifu wa mtu aliye rafiki yako fanya kwa uzuri huku ukitambua nawe ni dhaifu katika upande mwingine.
Unapo kuwa na rafiki yako lazima utambue furaha yake ndio burudiko lako na sivinginevyo, ni vizuri utambue anaye weka ni Mungu kwaiyo haina uhusiano na mtu kupenda au kuto penda.
Kama mtu athamini udhaifu wako jua kwamba mtu huyo hana shirika la kweli na wewe kwa kuwa unahitaji kuona namna anavyo onyesha upendo wake kwako.
Anayetambua kuona maana ya wewe kuwa katika hali iliyo njema haone maana yaw ewe kuwa rafiki yako.
                                             VIII.anayependa mshirikiane
Ni mtu anaye tambua uthamani wa uwepo wako japo inawezekana kufanya hata akiwa peke yake kwakua anatamani mfanikiwe kwa pamoja.
Pindi anapofanya shughuli yoyote pamoja na wewe anaona kuna kutiana nguvu na kufanya shughuli kwa ufanisi zaidi.
Mioyo yenu inatambuana katika yote mnayo shirikiana katika kufanya jambo ambalo mnashirikiana.
Uwepo wa mmoja wapo inakuwa chachu nzuri katika kufahamiana na kuonana katika utendaji wenu kwa ufasaha zaidi.
Huwa hamshirikiani kwa sababu mnatakiwa tu mshirikiane bali ni hali yenu ya ndani inakuwa na uhitaji huo, utendaji wenu unatawaliwa na furaha.
Hana ubinafsi ndani yake bali anafanya yote kwa moyo wa kupenda na huku akitambua kuwa wewe ndio yeye kwaiyo kama nafsi yake ilivyo ndivyo anavyo ona fahari juu yako.

Prepared by:
                    Cothey Nelson       -  0764 018 535 or Cotheyn@yahoo.com
                  
                    James Adili Katiti – 0713 398 042 or James.adili19@gmail.com
       
                 Rafiki mzuri kwa hatua bora ya maisha”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni